ISO 4217
Mandhari
ISO 4217 ni kifupisho sanifu cha pesa za nchi zote. Kimewekwa na Shirika la Kimataifa la Usanifishaji (kwa Kiingereza "International Organization for Standardization, ISO").
ISO 4217 ni orodha ya alama za vifupisho vya pesa. Kila kifupisho kina herufi tatu. Herufi mbili zinarejea nchi, na herufi ya tatu inarejea jina la pesa la nchi husika.
Kwa mfano,
- kifupisho cha pesa ya Japani ni JPY, yaani JP kwa Japani, na Y kwa Yen.
- kifupisho cha pesa ya Tanzania ni TZS, yaani TZ kwa Tanzania, na S kwa Shilingi.
- vivyo hivyo Kenya ina KES, yaani KE kwa Kenya, na S kwa shilingi.
- tofauti kwa sababu za mabadiliko ya kihistoria ni kifupisho cha pesa ya Uganda ni UGX, yaani UG kwa Uganda. X inaitaja shilingi mpya ya Uganda (tangu 1990). Hadi 1987 kifupisho cha ISO ilikuwa UGS kwa ajili ya shilingi ya kwanza iliyoharibika kabisa wakati wa utawala wa Iddi Amin na vita ya wenyewe kwa wenyewe iliyofuata, ikawa "old shilling" yenye kifupisho cha ISO UGW kwa kipindi cha 1989 to 1990 halafu tangu mwaka 1990 UGX pekee kwa shilingi mpya iliyokuwa sasa pesa halali ya pekee nchini Uganda.[1]
Orodha ya vifupisho vya ISO 4217
[hariri | hariri chanzo]Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ tazama List of codes for historic denominations of currencies & funds kwenye tovuti ya https://www.currency-iso.org, ilitazamiwa Mei 2017
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]| Makala hii kuhusu mambo ya uchumi bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu ISO 4217 kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |